Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri
Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo
amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka
vipaumbele vingi
visivyotekelezeka kwa wakati.
Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.
Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa
kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za
kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu
uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.
No comments:
Post a Comment